Habari Mpya

Powered by Blogger.

Videos

KITAIFA

KIMATAIFA

BIASHARA

KILIMO

HABARI PICHA

LEMA KUJITOSA KWENYE KAMPENI

Mhe. Godbless Jonathan Lema .

" Kampeni za Ubunge Arusha Mjini zinaanza kesho Novemba 5, 2015

Uchaguzi utafanyika Disemba 13, 2015

Bado tunapambania
#Mabadiliko
Tushirikiane kufanya mabadiliko makubwa katika Halmashauri yetu ya Jiji la Arusha. Tuna madiwani 24 kati ya 25 walioshinda kwenye Kata.

Tunatakiwa sasa kutetea nafasi yetu ya Ubunge kwa kura nyingi mno."HAYO YAMESEMWA NA WADAU WA UKAWA.


The Wrath Of Vajra


Unajua Thamani ya tofali moja ya Dhahabu ambayo ni kilo moja?Jihoji Mtanzania

Tujihoji kwanza hata kama una maslahi binafsi na ccm jiulize thamani ya Madini yetu na thamani unayaishi ukipata jibu ya kuwa tunahitaji mabadiliko,chukua hatua bila kuangalia na kusikia maneno ya wahujumu haki yako.

Rushwa hii ya Magufuli haitafautiani na ile ya Maisha Bora kwa kasi mpya.

Baada ya magufuli kusema pale dodoma kuwa hata waangusha wana ccm,kisha akasema anajua shida za watanzania,kisha akaja na Kutetea waendesha bodaboda na mama ntilie,alipofeli sasa amekuja na rushwa ya kugawa laptop kwa waalimu kwa maneno na kusambaza milioni 50 kila kijiji,hii inaonyesha udhaifu mkubwa wa magufuli na wapambe wake,ndiyo maana wamebakia na masengenyo ya kufitini mgombea wa Ukawa kwa kujionyesa kuwa wao ni wasafi wasiyo na hatia,wanasahau kuwa hao anaowadanganya ndiyo wanaomkataa,na hao wanao mchagua wanayemtaka ndio anaotaka kuwapa ahadi ya Rushwa ya maneno ambayo hayana mashiko,sisi wana wa kitanganyika na Zanzibar tunataka mabadiliko. Na Waalimu hawataki Laptops wanataka kuboreshewa maisha wathaminiwe kama wanasiasa walivyojikinai wanavyo jithamini hadi kufikia hatua ya kukatalia Ikulu,sasa ni wakati wa kuondoa ujinga na kuanza upya siyo wakati wa kudanganyana.Maisha ya bahadi ziliishia 2010 sasa ni mwendo wa kushoma na kufuta ccm ndiyo kauli ya waalimu.

Je! ni halali nchi kutumia Noti aina mbili?na kama ni halali kwanini mataifa mengine hawatumii?

Ni wazi kwamba nchi yetu imevamiwa na wahalifu ambao hutumia Nguvu za Giza kupumbaza watanzania wasione makosa yanayo tendwa na utawala uliok madalakani,tangu nizaliwe sijawahi kuona Nchi yeyote ikitumia noti aina mbili,ila kwa mara ya kwanza nimeiona Tanzania NA WANAOFANYA HAYA WAKO SALAMA WALA HAWANA WASIWASI.
Maisha yamepanda na suruhisho hakuna kwa wajisemeao kuwa ni viongozi wa taifa huku wanadidimiza nchi na kujiwekea wigo wa ulinzi kwa kutumia Dola,haki ya mwananchi kufanya maamuzi inauwawa na kupuuzwa ilimradi wenye madaraka wale na kujikinai wanavyotaka,noti zetu halali siyo hizi za utawala wa kikwete,ndiyo maana hata marekani  imewekea kikwazo moja ya Benk inayojihusisha na utakatishaji wa Pesa,moja wapo ya maswali tunayopaswa kujiuliza ni pamoja na kwanini noti mpya ni noti zinazolika,na hata zilipotolewa serikali haikufuta za zamani,hii imekula kwetu,na nawahurumia sana wanaoshabikia ccm ambayo imetupelekea umasiini na madeni ambayo i zaidi ya yale tuliyosamehewa miaka kumi iliyopita,Serikali haina pesa pesa wamebeba viongozi wa kisiasa za chama tawala,kitu ambacho kinaligarimu taifa hadi sasa waliyo fanya uhalifu wanatumia chuki kujisafisha na kuwafanya watanzania wasione uovu wao,wanausukuia ambao hawajawahi kuchukua Dola na wao kutumia pesa zetu kuua uchumi na kuhaibu maisha ya wananchi,huku wakiimba amani amani huku wanaua na kuharibu hazina za vizazi vijavyo.

Bodaboda wasema Kauli ya Magufuli ni maneno tu! kama Ahadi za JK

Foko news imekua ikipata habari za michanganuo mbalimbali ya vijana wengi maeneombalimbali kuhusiana na kauli za Magufuli aliyedai kuwa endapo kama watamchagua atahakikisha wasikamatwe na polisi,kitu ambacho makundi ya vituo mbalimbali wamesema Matrafiki huwakamata kwa lengo la kutekeleza mradi wa wakuu wao,kitu ambacho hakiwezi kuisha kwa kumpitisha Magufuli,mmoja akaeleza kuwa kama alijua kuwa akichaguliwa atawalinda huo utakui wake na wenzake kunyia makusudi ili wawaombe kura,nao wasema kwa muda wote huo kama walikuwa hawajaliona hilo wao wameafiki kuleta mabadiliko, ila kwa habari ya kuwakodi kupeleka makada wao mikutanoni wako teali maana wapo kazini,kama ni kura itakayo waondolea kukamatwa wasema hapo Magufuli aende na gia nyingine wenzake walisha kuja kwa ahadi ya maisha bora matokeo yake wamefirisi nchi.

Walipochukua Fomu wadaku hawakukosa la kusema

Wadaku katika medani ya kuuza magazeti na kutumiwa na wahujumu uchumi wa nchi,kitu ambacho kinawatafuna watanzania na hata hao wanaofanya udaku kupotosha watu kwa kuingiza taifa kwenye utawala wa kiduni na mikandamizo ya kimasikini,ambapo watanzania wengi wamekuwa watu wa kuwaza njaa badala ya maendeleo,na uduni huu umekuwa sehemu ya kudidimiza uchumi kwa kujimilikisha kifalme nchi ya watu zaidi ya mil 45 kitu ambacho kufikia miongo ijayo hakutakuwa na madini zaidin ya mashimo na watakao kuja hawata ambulia kitu,hatimae hata watakao kuja huenda wakawa wanakumbwa na majanga ya ardhi kubomoka kama maeneo ya Kahama,Geita,Mgusu,Nyamongo,Merelani,na sehemu zingine,je! hawa watu wa udaku wanao potosha wanajitazama wao tu! kwa kutetea wadharimu kujikinai kwa mali za kitaifa kitu ambacho kimepelekea taifa kukosa pesa na pesa zote kuhamishiwa mikononi mwa viongozi wa ccm.

SIRI YAFICHUKA LIPUMBA NI MCCM

Baadhi ya watanzania wamesema pamoja na Lipumba kudai katika hotuba yake kuwa hajaafiki Mtu aliye husika kutoleta katiba ya wananchi,ailete kwa kuhamia UKAWA kuileta katiba,wamedai kama angelikuwa mzalendo asingetoka nje ya bunge la katiba,na hata akisema kaanzisha ukawa ukawa imeanzishwa na wanaounga mkono katiba ya wananchi,ndiyo maana hata sasa ameshindwa kusimamia ukweli wake anaoudai kuwa yeye hajatendewa haki,ikumbukwe wazi kuwa yeye alikuwa mgombea wa CUF tangu 1995 akashindwa na hadi mwaka 2000 alisababisha mauwaji ya Watanzania wa Mwembe Chai na Pemba,Watu wakauwawa wasiyo na hatia kwa kua hata sasa ameisha fanya watanzania kuwa niwa jinga,nao wameisha msoma tangu aliposhawishiwa na ccm kujiunga na ccm,alinunuliwa kuidhoofisha CUF, na baada ya hapo upnzani wa CUF ukadhoofu,na kupitia hatua hizi baadhi ya wajuzi wa kisiasa waliona huyu ni adui wa mabadiliko,ndiy maana hata maandamano yake yalikuwa ya kuumiza wananchi na wengine kukamatwa maana alikuwa ni chambo cha kutumiwa na ccm kuhujumu CUF na kudhofisha upnzani,Lipumba alitumiwa na adui kupita kila kona waliko wapinzani wa kwenli na alisababisha mauwaji na wengine kukamatwa na kupelekwa mahakamani,yeye alikuwa mleta vurugu siyo haki. Waswahili wanasema lisemwalo lipo na kama halipo linakuja na hatimaye kajitoa kwa lengo la kuua mabadiliko ya Watanzania,wengi wasema siasa ya lipumba ni siasa ya kusaka tonge,akiisha kupokea tonge hukimbia,na sasa baada ya kupokea Rushwa amesaliti watanzania kwa kusingizia kuwekwa mtu asiyestahiri,je! yeye anastahili?maisha ya watanzania hupiganiwa na watanzania wenyewe,lipumba hata kama angepewa uongozi angeiuza Nchi.Huu ni wakati wa kufanya mabadilik bila kuangalia sura,hata adui waumbuke.

Timu iliyo pangwa Ukawa ni watu wenye uwezo wa kisaikolojia na kusimamia wanachokijua.

Uteuzi wa umoja wa Ukawa umekuwa Gumzo kwa watanzania kwa kuweka wagombea wachapa kazi ambao wote wanauwezo wa kusimama mahali palipobomoka pakatengenezeka,Foko News ikiongea na baadhi ya wataalam wa kisiasa wamesema huu ni uamuzi wa kuonyesha ukomavu wa kisiasa bila kuangalia ukabila na udini,kitu ambacho kilikuwa taabu sana kwa muda mrefu,wagombea hawa wameweka wazi mwonekano uliyo wasukuma kugombea Kuiongoza Tanzania ili kuleta mabadiliko ya katiba na kuondoa madhaifu yaliyo kuwa tatizo miaka mingi.

Lowassa akiwa katika hotuba asema oct/25 Ukawa itachukua Dola.


Asema kinachompa msukumo wa kugombea ni kuhusu kulitumikia watanzania, na Ukawa,anasema kila mwenyenia ya kugombea ni mwenye msukumo wa ndani wenye nia ya kujitolea kwa wananchi,na lazima kuwa na maamuzi magumu,kwa kuleta mabadiliko,ameweza kuwashukuru Ukawa na kuahidi kuwa tarehe Ishirini ni siku ya kuchukua Dola tena asubuhi,amesema sasa siyo safari ya matumaini sasa ni safari ya matumaini,amempongeza sana Mbatia,na kumpongeza Seifu na kusema kujiunga kwake na Seifu ni kuvunja muungano,yeye kasema hatavunja muungano,na wale wanao taka kukusanya pesa kwa kukimbia nchi wasiwe na wasiwasi,bali watulie,
Kuhusu amani amesema wanao sema Amani ya nchi itavunjika haita tokea bali itatokea kwao wenyewe.
Na umoja wa Ukawa kwa kujiamini na  baada ya hapo wanachadema na ukawa wameitikia kwa Nguvu na kuhakikisha kuwa watakuwa na ushirikiano,
Ameahidi kupita jimbo kwa jimbo na kuleta mabadiliko,amesema kazi mbele kwa mbele tukutane kwenye majimbo.

Mhe.Juma Duni Haji,Asema umasikini wa watanzania unafanywa kimakusudi.




Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Wananchi (CUF) ngazi ya Taifa na Waziri wa Afya wa Serikali ya Zanzibar, Mhe.Juma Duni Haji amepitishwa rasmi kuwa Mgombea Mwenza wa Mhe.Edward Lowassa kupitia CHADEMA. Hii ina maana Duni amejiuzulu dhadhifa zote ndani ya serikali na ndani ya chama chake CUF ikiwa ni pamoja na kujivua uanachama wa CUF na kupewa kadi ya uanachama ya CHADEMA. Amesema umasikini wa watanzania ni umasikini wa kimakusudi ili ccm iwatawale watanzania kwa urahisi,amesema hakuna unafuu wa maisha hata kwa waalimu ambao ni kiungo mhimu cha watanzania na dunia nzima,amegusia madai ya adactari wanao daihaki yao na kupigwa mabomu,ameomba wana usalam wajali wana nchi huku wakijua kuwa wananchi ndiyo wanao wafanya kula lakini wanawaua kwa mabomu,ameongeza kusema kuwa umoja wa ukawa ni sehemu ya mabadiliko na wakati ni sasa kuanzia ndani ya familia zetu na hatimaye kuleta mabadiliko.

Uwezekano wa kuzuia goli la mkono Ni mkubwa,na Lowassa atapeperusha Bendera.

Wakati mheshimiwa Lowassa akiwekwa rasmi Ukawa,uwezekano wa kuzuia Goli la mkono upo,maneno hayo yamewekwa wazi na Halima Mdee,kwa kujiamini na maneno hayo yamegusa wengi na kuonyesha matumaini makubwa ya ushindi kwa kile alicho sema kuwa Chizii mwenyewe tunaye,na hii imeonesha umakini wa umoja wa Katiba ya wananchi,uhakika unaojengwa na umoja huo ni kuleta mabadiliko nchini,kitu ambacho kitaondoa madaraka ya mabavu dhidi ya wananchi.

Milca Kakete Aingiza sokoni album zake Mbili kwa mpigo.

Mwimaji wa music wa Injili aishiye Canada Milca Cakete,baada ya kufanya ziara Tanzania na Kenya sasa ameachia album zake mbili rasimi,ambazo ni NATAMANI,naNAKUNG'ANG'ANIA,zinapatikana madukani katika maduka ya kuuza nyimbo za waimbaji wa Injili kenya na Tanzania.